Siyo busara kiafya
Kati ya mambo ambayo si busara kumtangaza mwenzi wako, ni kuwa mliachana kwa sababu hazai, tena ukaongeza na maneno machafu juu.
Kupata uzazi si kwa ujanja wa mtu bali kwa mapenzi ya Mola.
Kuna kujisifu umezaa ila uzao wako ukakoswa baraka, mwishowe ukaishia kuwa na watoto wengi Alhamdulillah ila wote hawana elimu ya utambuzi yaani vichaa, teja, wenye kuishia gerezani n.k yaani wasikufae kitu
Ndoa ikikosa watoto isiwe chanzo cha kukufuru, kaeni pande zote mbili na elezeaneni bayana ili muachane kwa amani au mnaweza kuendelea kuwa pamoja hata kwa mtoto wa kuwasiri yaani adoption au mume akaamua kuongeza mke wa pili (kama imani inaruhusu) kwa ajili ya kuongeza nasaba
Maoni
Chapisha Maoni